Kwa wasiofahamu, Whatsapp ni moja ya programu za simu za mkononi
inayokuwezesha kutuma ujumbe wa simu kupitia kwenye Intaneti badala ya
ujumbe mfupi (sms). Kwa kutumia Whatsapp, ina maana utaepuka gharama za
sms huku ikiwa imesheheni matumizi mengine mengi zaidi kama kutuma
picha, sauti uliyojirekodi, nk.
Hadi sasa, Whatsapp ina watumiaji hai milioni 450 kila mwezi kutoka
nchi nyingi duniani, huku kukiwa na watumiaji wapya zaidi ya milioni
moja kila siku. Hivyo, ni dhahiri kuwa Whatsapp ni programu pendwa na
yenye kutumika.
Whatsapp inaweza kutumika kama njia rahisi zaidi ya mawasiliano kwa
watu binafsi na hata makampuni