NDOA YA JIDE KUVUNJIKA GARDNER AFUNGUKA.

 
Staa wa muziki wa Kizazi Kipya, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ au ‘Jide’ akiwa na  mumewe Gardner G. Habash wakati wa harusi yao.

HABARI kubwa ya mjini hivi sasa, hasa kwenye mitandao ya kijamii ni juu ya madai mazito ya kuvunjika kwa ndoa ya selebriti wawili Bongo, staa wa muziki wa Kizazi Kipya, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ au ‘Jide’ na mtangazaji maarufu wa Radio Times FM, Gardner G. Habash, iliyofungwa Mei 14, 2005, Ijumaa linamaliza utata.
KABLA
Kabla ya Gardner kufunguka, habari zilidai kwamba wawili hao walikuwa kwenye gogoro zito ambapo Gardner aliamua kuondoka katika nyumba waliyokuwa wakiishi pamoja iliyopo Kimara-Temboni, Dar.
Ilidaiwa kwamba baada ya kuondoka nyumbani eti Gardner alikwenda kukaa kwa mmoja wa ndugu zake.

Habari hizo za kwenye mitandao ambazo hazitaji chanzo cha kuvunjika kwa ndoa hiyo, zilidai watu wa karibu na familia hiyo walisema hiyo siyo mara ya kwanza kwa wawili hao kutengana, lakini mzozo wa safari hii unaweza ukawa wa moja kwa moja.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...