STAA wa muziki na filamu Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amewachana wasanii wanaojihusisha na madawa ya kulevya kuwa ni wavivu.
“Wanafikiri mafanikio yanakuja kirahisi bila kujishughulisha, ninawashangaa sana kwani wanajishushia hadhi zao kwa tamaa ya kutaka kuwa na maisha mazuri bila kufanya kazi, badilikeni,” alisema Shilole.