WAZIRI AJIUA BAADA YA KUSHINDWA UCHAGUZI


Waziri wa serikali za mitaa nchini Malawi, Godfrey Kamanya, amejiua baada ya kushindwa katika uchaguzi mkuu siku ya Jumanne.
Waziri huyo alijipiga risasi nyumbani kwake baada ya kupata taarifa za kushindwa.
Matokeo ya kura bado hayajatangazwa rasmi katika kile kinachosemekana kuwa uchaguzi wenye ushindani mkali sana.
Afisa mkuu wa uchaguzi, amesema kuwa mfumo wa elektroniki umeharibika na maafisa wanatumia matokeo kwa njia ya barua pepe.
CHANZO BBC SWAHILI


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...