UWANJA WA AZAM WAPEWA KIBALI NA CAF KUTUMIKA KWA MECHI ZA KIMATAIFA

 
Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika CAF leo tarehe 31 Januari 2014 limeupa kibali 
cha kuchezea  mashindanoya kimataifa yanayoandaliwa na CAF uwanja wa Azam Complex Chamazi na kuufanya uwanja  
wa kwanzaunaomilikiwa na klabu Afrika Mashariki  kuruhusiwa kuandaa (ku-hostmashindano makubwa ya 
vilabu
Kwa mujibu wa barua pepe iliyotumwa leo na CAF kupitia kwa naibu mkurugenzi wa mashindano Bwana  
KhaledNassarUwanja wa Azam Compex Chamazi umepita vigezo vyote vinavyohitajika na CAF “ku-host”  
mashindano yakimataifa hivyo kuanzia tarehe ya leouwanja huu unaruhusiwa “ku-host” mech za CAF
Bwana Khaled ameandika katika taarifa yake ya barua pepe kwenda TFF na Azam FC kuwa CAF ilimtuma  
mkaguziwake toka nchini Zimbabwe Bwana Wilfried Mukuna kuja kukagua uwanja huuBwana Mukuna  
aliwasilisha ripotiCAF iliyopelekea shirikisho hilo kutoa kibali kwa Azam FC na TFF kuruhusiwa kuutumia  
uwanja huu kwa mechizinazoandaliwa na CAF
Uongozi wa Azam FC unatoa shukrani kwa mkaguzi wa CAF Bwana Mukuna, Uongozi wa TFF chini ya Rais JamalMalinzina uongozi wa CAF Cairo Misri hasa Bwana Khaled Nasser  
kwa kuwezesha zoezi hili kufanyika kwa uwazina uweledi wa hali ya juu uliopelekea uwanja wetu kupata  
kibali cha kutumika kwenye michezo ya kimataifa.
Azam FC ingependa kuwataarifu wapenzi wake kuwa kuanzia msimu huu mechi zake za  CAF zitachezwa  
AzamComplex Chamazi


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...