AJALI YA PIKIPIKI:. WANAFUNZI 2 WA CBE DODOMA WAPOTEZA MAISHA

Asikari wa wa usalama barabarani wakipima upana wa barabara sehemu ilipotokea ajali hiyo.
Baadhi ya watu wakiisogeza miili ya Wanafunzi wa CBE Dodoma  waliopoteza maisha kutokana na kuligonga tela la lori kwa nyuma.
Asikari wa Jeshi la wananchi walionekana kujaribu kutoa msaada katika ajali hiyo.

WANAFUNZI wawili wa Chuo cha biashara(CBE ), Dodoma wamepoteza  maisha papo hapo kwenye ajali baada ya kugonga tela la mizigo lililokwama barabarani baada ya kuhalibika.
Ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa 1.00 usiku baada ya kugonga tela la lori la mizigo kwa nyuma wakati wanafunzi hao walipokuwa wakitokea kwenye mwaliko wa sherehe ya rafiki zao iliyofanyika katika kijiji cha ihumwa manispaa ya Dodoma.
Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma Suzan Kaganda alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa wanafunzi hao wakati wakiendesha pikipiki hiyo  yenye namba za usajili T420CCN  waliokuwa wakitokea barabara ya morogoro kuingia mjini.Suzan aliwataja kuwa ni Ramadhan Lesso na Gerger Lwandala wanafunzi wa CBE  na kwamba uzembe wa Dereva wa lori hilo lenye namba za usajili T 477 ABM na huku Tela lake ni T 838 AAZ aliyeliacha barabrani zaidi ya wiki bila kuweka alama yoyote huku matengenezo ya barabara hiyo yakiendelea katik eneo hilo.


Picha Na John Banda, Dodoma


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...