MSANII WA BONGO MOVIE ASIMULIA ALIVYO HONGWA TSH MILION 5 ILI AFANYE MAPENZI KINYUME NA MAUMBILE.


Msanii anayeuza nyago kwenye filamu za
Kibongo, Coletha Raymond ‘Koleta’
amefunguka kuwa analaani mastaa
wanaokubali kutumiwa kimapenzi kinyume na
maumbile akidai kuwa wapo ambao
wamekuwa wakifanya kitendo hicho kwa tamaa
ya pesa.
Akiongea  na gazeti la Ijumaa, Koleta alisema
anachukizwa na tabia hiyo kwani ni uchafu na
kujidhalilisha kulikopitiliza.
“Wanaume siku hizi ni matapeli sana, wengi
wanataka kuwatumia wanawake kinyume na
maumbile hivyo wasanii wa kike tuwe macho.
Alishawahi kunitokea mwanaume mwenye
heshima zake, alinipigia simu na kuniambia
licha ya kuwa na mke kuna vitu anavikosa.
“Nilipomuuliza ni vitu gani akaniambia anataka
anitumie kinyume na maumbile na nichague
zawadi isiyopungua milioni tano aniletee,
nikakataa na kumwambia sifanyi biashara
hiyo, ukweli mimi nakemea na ninawachukia
sana wanaofanya mchezo huo,” alisema
Koleta.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...