WAZIRI MKUU FINLAND ATEMBELEA BANDARI YA DSM.


 Waziri mkuu wa Finland Jyirk Katainen ameingia katika siku ya pili ya ziara yake ya kikazi nchini Tanzania kwa kutembelea bandari ya Dar es Salaam na kuongeza kuwa nchi yake pamoja na umoja wa ulaya inaunga mkono mpango wa serikali wa matokeo makubwa sasa na kwamba bandari za kisasa zinazotoa huduma kwa wakati ni muhimu katika kuchochea uchumi wa nchi yeyote duniani.
Ni siku ya pili ya kuwepo kwake hapa nchini Tanzania waziri mkuu wa Finland Jyirk Katainen ambapo katika siku hii anatembelea bandari ya Dar es Salaam ili kujionea hali halisi ya bandari hiyo na baadae kupata fursa ya kuzungumza na baadhi ya viongozi wa serikali na watendaji wa bandari ya Dar es Salaam.
Akizungumza na viongozi hao mara baada ya kutembezwa bandarini hapo waziri mkuu huyo pamoja na mambo mengine amesema kuwa nchi yake pamoja na bara la ulaya inaunga mkono Tanzania katika mpango wake wa matokeo makubwa sasa katika sekta ya miundo mbinu ikiwa ni pamoja na kuiboresha bandari ya Dar es Salaam na kuongeza kuwa bandari za kisasa zinazotoa huduma kwa wakati ni kichocheo kikubwa cha ukuaji wa uchumi.
Akizungumza katika mkutano huo balozi wa umoja wa ulaya hapa nchini Mh Filiberto Sebregondi amesema kupitia mpango wa serikali wa matokeo makubwa sasa tayari mabadilko yameanza kujidhihirisha katika bandari ya Dar es Salaam na kwamba jitihada zaidi zinahitajika ili kuiwezesha bandari hiyo kupokea na kusafirisha bidhaa nyingi zaidi.
Kwaupande wake waziri wa uchukuzi wa Tanzania Mh Harrison Mwakyembe ameitumia fursa hiyo kumueleza waziri mkuu huyo matokeo ya mkutano wa jukwaa la kimataifa la uchumi uliofanyika hivi karibuni Davos nchini Uswis kuwa katika miradi 51 iliyowasilishwa katika mkutano huo kwa ajili ya kupewa kipaumbele na kuendelezwa kama mfano wa ushiriki wa sekta binafsi katika miradi ya miundo mbinu barani Afrika mradi wa ukanda wa uchukuzi wa kati ulioko Tanzania umeteuliwa.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...