MBUNGE WA CHADEMA AZICHAPA NA MKURUGENZI WA HALAMASHAURI YA WILAYA LIVE !!

Mbunge wa Chadema, Paulina Gekul.
Arusha, Tanzania. Mbunge wa Viti Maalumu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoani Manyara, Paulina Gekul LEO, ameshambuliwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Babati, Omari Mkombole na mbunge huyo kulazimika kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi ambao wameingilia kati sakata hilo.



Katika vurugu zilizotokana na Mbunge wa Chadema kupigania maslahi ya Wananchi, pia Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mohamedi Fara naye ameshambulia wakati wakigombea kabrasha lenye majina ya wananchi wanaopaswa kupewa ardhi.


Katika pukurushani hizo Gekul amesema amechaniwa nguo zake, na kwamba amedhalilishwa na kuporwa fedha zaidi ya Sh5 milioni zilizokuwa kwenye mkoba wake.

Vurugu hizo ziliibuka baada ya kumalizika kwa kikao kilichofanyika chini ya mkurugenzi huyo kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Babati.

Baada ya mbunge huyo kushambuliwa alikwenda polisi kutoa taarifa za kushambuliwa na vigogo hao wa halmashauri na kuweka wazi kuwa kiini cha vurugu hizo zilitokana na kikao cha kujadili ugawaji wa shamba la Sisal Plantation lenye ekari 4200.

Vyanzo vya habari vimebainisha kuwa awali vigogo hao wa halmashauri hiyo walimpokonya nyaraka ambazo walidhania zilikuwa na majina ya wananchi ambao wanatarajiwa kugawiwa viwanja, lakini walipobaini karatasi au nyaraka walizpora hazina majina ya wananchi hao walimfuta huku akijaribu kutoka nje na kumfungia ndani ya ukumbi wa Babati na kumpora pochi yake na kutoa nyaraka pamoja na kuchukua fedha.

Chanzo kingine kimebainisha kuwa awali wakati kikao hicho kikiendelea inasemekana mbunge huyo alibaini katika nyaraka ambazo zimekusudiwa na halmashauri kutumika wakati wa kugawa shamba hilo zilikuwa zimechomekewa majina ya maofisa mbalimbali na kuwaacha wananchi wengi bila kuwapo kwenye mpango wa mgao huo.

Taarifa zinaeleza baada ya mbunge huyo kuonekana kushtukia mchezo huo ndiyo vigogo wa halmashauri walifunga mlango na kumpora nyaraka hizo.


Imeelezwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Babati wakati akizungumzia sakata hilo amesema mtu yoyote amempiga mbunge huyo.
Kuhusu, Mkurugezi wa Halmashauri hiyo hajasema lolote mpaka sasa licha ya waandishi wa habari kumtaka atoe maoni yake kuhusu sakata hilo.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...