ATHARI ZA MGOMO WA DALADALA MANISPAA YA MORO

Wanafunzi wa shule mbalimbali za Manispaa ya Morogoro wakisubiri usafiri wa kwenda shule bila mafanikio katika kituo cha mabasi kilichopo Mkoani Morogoro.
Wanafunzi wa shule mbalimbali za Manispaa ya Morogoro wakiwa kwenye lori baada ya mgomo wa madereva daladala leo.
...Baadhi yao wakizidi kusubiri usafiri.
...Baadhi ya wanafunzi wakishuka baada ya kufika wanapoelekea.
Mmoja wa madereva wa daladala Manispaa ya Morogoro, Bw. Ramadhani Shukuru akiongea na wanahabari.
MADEREVA wote wa daladala Manispaa ya Morogoro leo wamegoma kutoa huduma ya usafiri wakilalamikia kukamatwa hovyo na maafande wa Kikosi cha Usalama Barabarani katika manispaa hiyo.
Akizungumza na tovuti hii, mmoja wa madereva wa daladala hizo, Bw. Ramadhani Shukuru alisema kwamba kwa siku gari linakamatwa mara mbili na kwamba ukifikishwa kituoni unalipishwa faini ya shilingi 90,000/=
"Unakamatwa asubuhi unalipa 90,000/= makosa matatu, ukiachiwa na kuanza kazi ukifika Kihonda unakamatwa tena ukijitetea askari anakwambiaa yeye hausiki na kukamatwa kwako kwani amekukamata kwa makosa mengine unaenda tena kituoni wanakukamua 90,000/= nyingine kesho unakamatwa tena, sasa si bora tuegeshe magari tukalime matombo!" alisema Rama.
(PICHA ZOTE NA DUSTAN SHEKIDELE / GPL, MOROGORO)


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...