DEREVA ANUSURIKA KIFO ARUSHA BAADA YA GARI LAKE KUSOMBWA NA MAFURIKO AKIWA ANALIENDESHA

Baadhi ya wasafiri na wanakijiji wakitizama daraja la Kirurumo lililoharibiwa kwa mafuriko na kukata mawasiliano kati ya Karatu, Ngorongoro na Serengeti.
Mamia ya wasafiri waliokuwa wakitokea Karatu kuelekea Arusha, Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi, wameshindwa kuendelea na safari baada ya kushindwa kuvuka mto Kirurumo uliopo mpakani mwa Wilaya za Karatu na Monduli, baada ya mto huo kufurika na kufunika barabara kutokana na mvua za masika zinazoendelea kunyesha.
  
Mwandishi wa habari wa TBC aliyeko Manyara ameripoti kuwa miongoni mwa watu waliokwama ni pamoja na watalii waliokuwa wakitoka katika hifadhi za Taifa za Serengeti na Ngorongoro, na abiria waliokuwa wakisafiri kwa basi la Dar Express ambalo lililazimika kurejea mjini Karatu kwa kushindwa kuvuka mto huo.
  
Abiria wengine waliokuwa wakisafiri kwa basi la Sai Baba kuelekea jijini Dar es Salaam nao hawakuweza kuendelea na safari yao kutokana na marufiko hayo.
 
Mto huo umekuwa ukiporomosha mawe makubwa kutoka milima ya Mbulu Mbulu
Dereva wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Juma Mushi, ameponea chupu chupu kupoteza uhai katika mafuriko hayo, baada ya gari aina ya Toyota Land Cruiser SU 36037 kusombwa na mafuriko hayo katika mto Marera, nje kidogo ya mto wa Karatu, na kukokotwa kwa umbali wa kilometa 70 kutoka barabarani. 
Katika jitihada za kujiokoa, dereva huyo alilazimika kutoka kwenye gari lake na kupanda juu ya mti.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...