BAADA YA KUZUNGUSHWA NA DAWASCO WANANCHI WA MWENGE NYUMA YA MAGHROFA YA JWTZ WAAMUA KUJITOA MUHANGA NA KUSHIKA KINYESI KUZIBUA CHEMBA ZA MAJI TAKA




Mmoja wa wakazi wa mtaa huu aliyeamua kujitoa na kushika kinyesi ili apate kuzibua chemba ambayo ilikuwa inamwaga maji bila kusimama kwa siku sita.
Hali hii ilikuwa mbaya jambo ambalo wananchi waliamua kujitolea na kufanya wawezalo ili kuzibua.
Hali ni tete eneo hili ambapo sasa moja ya chemba inazidi kumwaga maji. Hapa kila mtu anatoa wazo lake nini kifanyike ili kuweza kuzibua eneo hilo ambalo maji yake yalikuwa hayapungui kumwagika bali kuongezeka na mwisho wote waliona bora washike kinyesi kuliko kuendelea kuteseka.
Ilikuwa ni baada ya kuhangaika sana wakazi wa eneo hili kwa kutumia nyenzo yao duni ya nondo maalumu ya kuzibulia chemba waliyojinunulia wenyewe, hatimaye walifanikiwa kuzibua chemba moja na kuhamia chemba ya pili.
Baada ya chemba ya juu kuzibuka, kasheshe ikahamia katika chemba ya pili ambapo sasa maji yote yalihamia hapo.
Masikini mtazame mama huyu alivyoruka juu na mtoto akiwa amemshika kihatari namna hii.  Hii ni adha ya haya maji taka.
Wakazi wa eneo hili wakiwa wanakomaa kwa nguvu zote kuanza kuzibua chemba ya pili.
Zoezi sasa linaendelea na hapa walikuwa wanaendelea kuzibua chemba ya 3 ambapo walifika kikomo baada ya kuonekana chemba hiyo ilikuwa imejaa matakataka ya kutosha pamoja na mchanga. Ndipo walipopata taarifa kuwa DAWASCO wanakuja.
Wakiwa wamefika kabisa na kujionea adha ya kukanyaga maji taka.
Wafanyakazi wa DAWASCO wakiwa wamefika katika eneo la tatizo na kuanza kuzibua chemba za maji taka ili kuwasaidia wakazi hao wasipatwe na magonjwa.
Wakiwa wanahakikisha kabisa kwamba tatizo limekwisha eneo hilo.
Mojawapo ya chemba ambayo wakazi wa Mwenge walikuwa wamehangaika nayo sana mpaka kufanikiwa kutoa maji taka hayo yaende ikiwa inaangaliwa na wafanyakazi wa DAWASCO.
Wafanyakazi wa DAWASCO wakiwa wanaendelea kutoa takataka katika chemba sugu ili kuruhusu maji yapite.
Hii ni baada ya chemba kuzibuliwa na wananchi wakishirikiana na DAWASCO ambao walichelewa kufika eneo la tukio.
Maji yakionekana yanaendelea kukauka baada ya chemba hizo kuzibuliwa.
Hizi ni takataka zilizobakia baada ya kuzibuliwa chemba hizo.
Wananchi mtaa wa Mwenge waandamana na kufanya usafi kufuatia kero kubwa ilyokuwa sugu na hatari kwa afya zao, kero hiyo ikiwa ni kuziba na kufumuka  kwa chemba zinazopitisha maji machafu maarufu kama (majitaka).
Ikiwa nizaidi ya wiki mbili wakazi na watumiaji wa njia ya Mwenge katika mtaa huo uliogeuzwa jina na kupewa jina mahususi na mazingira ya mtaa ambalo ni mtaa wa (kinyesi street) wamekumbwa na kero ya kufumuka kwa chemba za maji taka na kuwa na harufu mbaya  hivyo wananchi wamehofia afya zao na kuanza kuzibua chemba za maji hayo huku kila baada ya mwezi huletewa bili na kuweza kuzilipia bila ya wasiwasi. Lakini kibao kimegeuziwa kwa wananchi kuwa ndio wamiliki wa shirika la maji safi na taka (DAWASCO) baada ya kuamua kuondoa adha hiyo iliyodumu kwa muda mrefu bila ya ufumbuzi kwa kushika kinyesi na maji machafu kutoka sehemu mbalimbali.

Hata hivyo wakazi walilalamika kuhusu utendaji kazi wa DAWASCO kuwa ni mbovu kwa kuwa wamewatafuta zaidi ya mara kadhaa  bila mafanikio.

Aidha wananchi walionekana kuwa na moyo mmoja wa ushirikiano kufuatia harufu mbaya iliyokuwa ikitoka katika chemba hizo na kufanikisha kuzibua chemba zote katika mazingira magumu yanayoweza kusababisha maradhi mbalimbali kwa jamii husika.
(PICHA NA DAR ES SALAAM YETU)


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...