MVUA YAKIHARIBU KITUO CHA MABASI NJOMBE, KERO YAWA KUBWA KWA WATUMIAJI‏


Baada ya mvua kubwa kunyesha jana mkoani Njombe, kituo hiki cha Njombe kimegeuka matope matupu na kusababisha watumiaji kupata tabu ya kutembea kwa shida na kutafuta eneo la kukanyaga ili wapite.
Hali halisi kutoka kituo cha mabasi Njombe.
Abiria ambaye jina lake halikujulikana mara moja akipita kwenye matope yaliyosheheni kwenye kituo hicho cha mabasi Njombe.
Ni mwendo wa kuchagua eneo la kukanyaga, wengine wanapandisha suruali zao juu zisipate matope.
Uenda upande huu una afadhali kwa abiria hawa lakini wapi, tope kila mahali.
Tope lenyewe.
LICHA ya tabu hii inayowakumba watumiaji wa kituo cha mabasi Njombe, ushuru umekuwa ukikusanywa kama kawaida, lakini miezi michache iliyopita Halmashauri ya Njombe ilitangaza kuwa haina mpango wa kukikarabati kituo hicho na badala yake imetenga eneo lingine kwa ajili ya kujenga kituo kipya cha mabasi.
Eddy Blog inaamini kuwa hii adha itaendelea kuwakumba wananchi na watumiaji wa kituo hiki kwa pamoja hivyo kwa kauli ya halmashauri inabidi abiria hao wazidi kuwa wapole na kuvumilia hali hii mpaka kijengwe kituo kipya!
(Picha na Eddy Blog)


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...