KABURI LA SHEIKH YAHAYA HUSSEIN LAVUNJWA, TAZAMA PICHA HAPA LIVE

Kaburi la Shekhe Yahya Hussein amezikwa tarehe 21.5.2011.
Kaburi la Sheikh Yahya Hussein ambaye alizikwa tarehe 21.5.2011.
Makaburi mawili ya Sheikh Yahya Hussein na Sheikh Kaseem Bin Jumaa yamevunjwa na mgambo wa jiji saa nane usiku eneo la Tambaza, makaburi ambayo yana muda mrefu katika eno hilo.

Hata hivyo haijajulikana chanzo cha kuvunjwa kwa makaburi hayo.
Wakiongea na Taarifa News baadhi ya wafanyabiashara wa maduka ya vyakula eneo hilo wamedai kuwa, walifika asubuhi na kukuta hali hiyo ya kuvunjwa kwa vibaraza vya maduka yao pamoja na kuvunjwa kwa makaburi hayo mawili ya watu masheikh mashuhuri hapa nchini.
Kaburi la Shekhe Kasimu Bin Juma amezikwa mwaka 1994
Kaburi la Sheikh Kaseem Bin Juma ambaye alizikwa mwaka 1994.
Naye mtoto wa marehemu Sheikh Yahya Hussein, Bi. Mariam Hussein alifika katika makaburi hayo na kujionea kwa macho yake jinsi kaburi la Baba yake lilivyobomolewa.
Mariam amesema anasikitishwa sana kwa kuvunjwa kwa kaburi la Baba yake bila ya sababu ya msingi.
Mtoto wa Marehu Shekhe Yahya Mariam Yahya Husein akitafakari jambo kwenye eneo alilozikwa Baba yake Mzazi.
Mtoto wa Marehem Sheikh Yahya Hussein,  Mariam Yahya Hussein akitafakari jambo kwenye eneo
 alilozikwa Baba yake mzazi. Picha na Mariam Mkumbaru.

Credit:
TAARIFA NEWS


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...