MH! Kigauni kifupi alichotinga staa wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe katika hafla ya chakula cha usiku iliyoandaliwa na Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ kimeibua minong’ono watu kuhoji kulikoni akivae hivyo ndani ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Tukio hilo lilowastaajabisha wengi lilijiri wikiendi iliyopita katika Mgahawa wa Great Wall uliopo Masaki, Dar ambapo asilimia kubwa ya waalikwa katika hafla hiyo walisema hakikustaili hasa kwenye mwezi huu wa toba.
“Achana nao hao ni wanafiki tu kwani kuna mtu amekatazwa kuvaa kama hivi?”