JACK WOLPER ADAIWA KUTIBUA UCHUMBA WA NAY WA MITEGO NA SIWEMA


Mwanamuziki Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ amefungukia madai ya kutoka na msanii wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper na kudai kuwa wao ni washikaji tu ila ukaribu wao umesababisha mtifuano kati yake na mchumba wake, Siwema.Akizungumza na mwandishi Nay alisema, watu wamekuwa wakieneza kuwa yeye na Wolper wanatoka kiasi cha kumkosesha amani Siwema na kufikia wakati f’lani wakatibuana.

 Mahojiano kati ya mwandishi wetu na Nay yalikuwa hivi: 

Mwandishi: Kuna madai kuwa wewe unatoka na Wolper, hii ikoje? 
Nay: Wolper ni mshikaji wangu, kama watu wanavyojua kwamba yule ana mambo ya kisela f’lani na hicho ndicho kinanifanya nimpende. 
Ila najua kitu kilichowafanya watu wahisi kuna kitu kati yangu na yeye ni baada ya kuposti picha yangu kwenye ukurasa wake wa Insta na hapo ndipo likaibuka tatizo. Na hilo lilileta ugomvi kwenye uhusiano wangu lakini ukweli ni kwamba kama mahusiano yapo ni ya kawaida tu.
Mwandishi: Sasa wewe na Wolper mkikutana huwa mnazungumzia nini?
Nay: Mambo ya kazi tu, si unajua nina mpango wa kucheza muvi baadaye

Mwandishi: Mbona sasa inadaiwa mnatoka kwa siri?
Nay: Hayo maneno ya watu tu japokuwa ni mwanamke mzuri, anamvutia mwanaume yoyote rijali
 
Mwandishi: Ikitokea ameingia mzimamzima kwako itakuwaje? 
Nay: Ikitokea ameamua kuingia mzimamzima, nitaangalia mapokeo yake (Kicheko sanaaa)

Mwandishi  alifanya jitihada za kumsaka Wolper kupitia simu yake ya mkononi lakini hakuweza kupatikana. 

Credit:Ijumaa/Gpl


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...