CHUCHU HANS AZIDI KUMUUMIZA JOHARI....AVAA JEZI YA RAY KIGOSI

STAA wa filamu Bongo, Chuchu Hans amedhihirisha kwamba ana mahaba niue kwa mpenzi wake, Vincent Kigosi ‘Ray’ kwa kulinadi jina lake hadharani kwa kuvaa t-shirt iliyoandikwa; ‘Ray Kigosi’.
Staa wa filamu Bongo, Chuchu Hans akiringisha chata la msanii Mwenzake, 'Ray'.
Tukio hilo lilichukua nafasi wikiendi iliyopita kwenye Tamasha la Usiku wa Matumaini lililofanyika katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar ambapo mwanadada huyo aliambatana na mashosti zake kushuhudia burudani tofauti ikiwemo mechi ya timu ya Bongo Fleva na
Movies anayoichezea mpenzi wake

Chuchu Hans akipozi.
Chuchu alivaa t-shirt ya njano ambayo mgongoni ilikuwa imeandikwa Ray Kigosi kitu ambacho hakuwahi kukifanya kabla.“Sioni tatizo kujinadi hadharani, atakayemaindi shauri yake, nafanya kitu roho inapenda bwana sijali maneno ya watu hata kidogo,” alifunguka Chuchu.usiku wa matumaini 2014


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...