Home »
Uncategories »
BABY MADAHA ANASWA LIVE NA BWANA WA WEMA SEPETU...!!NI YULE YULE WA NAIMA...!!!
BABY MADAHA ANASWA LIVE NA BWANA WA WEMA SEPETU...!!NI YULE YULE WA NAIMA...!!!
Unknown
11:24 AM
MSANII wa filamu na muziki Bongo, Baby Joseph Madaha hivi karibuni alinaswa nyumbani kwa kigogo anayetoka na Wema, Clement.Kwa
mujibu wa chanzo kilichoomba hifadhi ya jina lake, tukio hilo lilitokea
hivi karibuni ambapo staa huyo wa filamu na muziki alionekana akiingia
kwa usafiri wa teksi nyumbani kwa kigogo huyo anayeishi maeneo ya
Mwananyamala-Gereji, Dar.
Baada ya kujiridhisha na maelezo ya sosi huyo, mapaparazi wetu walimtafuta Baby Madaha ili kujua ukweli wa jambo hilo.
“Kweli nilikwenda hapo (kwa Clement), mimi sijui kama niliyeenda kuonana
naye ni bwana wa Wema kwa sababu sijawahi kumuona naye na nilimfuata
kwa ajili ya kuzungumza mambo ya kikazi,” alisema Baby Madaha.