ASKARI WANNE WA JESHI LA POLISI WAFUKUZWA KAZI KWA KWA KUJIHUSISHA NA VITENDO VYA UHALIFU

Kamanda  wa kanda maalum ya Dar es salaam  Kamishina Suleman Kova akizungumza na wanahabari muda huu ofisini kwake juu ya kufukuzwa kwa askari hao.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewafukuza kazi kwa fedheha askari wanne wa Jeshi la Polisi kutokana na makosa ya kujihusisha na vitendo vya uhalifu. Askari waliofukuzwa wanatoka katika vikosi mbalimbali kama ifuatavyo:
·    
E.6396 CPL RAJABU MKWENDA @ UGORO wa Makao Makuu ya Polisi.
·       F.9412 PC SIMON wa Kituo cha Polisi Kati.
·       F.9414 PC ALBERNUS  KOOSA wa Kikosi cha Bendi ya Polisi D’Salaam
·       F.9512 PC SELEMAN wa Kituo cha Polisi Kigamboni
Uchunguzi wa awali umeonyesha kwamba askari hao wamekuwa wakijihusisha na uhalifu ikiwa ni pamoja na tukio la tarehe 09/03/2014 eneo la Mbezi Beach “A” ambapo majambazi wapatao  15 walifika katika ofisi ya Kampuni ya Kichina ijulikanayo kwa jina la HONG 
YANG inayojishughulisha na ujenzi na uselemala.
Katika tukio hilo majambazi wapatao 11 wakivamia ofisi hiyo majira ya saa 04:30 Asb, na kupora vitu mbalimbali ikiwa ni pamoja fedha taslim, simu, n.k. na kutoweka. SOMA ZAIDI


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...