BREAKING NEWS: MVUTANO MAKALI BUNGENI BUNGE LIMEAIRISHWA

sita
Bunge Maalum  la Katika Limekutana Jioni Hii kuendelea na Shuguli zake Lakini Mvutano Mkubwa Umejitokeza Hali iliyosababisha Vurugu Kubwa Iliyoambatana na Kuzomea Zomea,Mvutano Huo Uliibuka  Pale Mjumbe Tundu Lissu Aliposimama kuomba Muongozo Kuhusu Marekebisho ya Kanuni Ambayo Tundu Lissu anamtuhumu Mwenyekiti wa Bunge Hilo Kupitia Kamati ya Uongozi kuleta Marekebisho Kinyume cha Kanuni zilizopitishwa na Bunge Hilo la Katiba.
Mwenyekiti wa Bunge Hilo Mh Samwel Sitta Aliingilia Kati kujaribu Kutoa Ufafanuzi  Pamoja na Wajumbe Wengine Akiwemo Mwanasheria Mkuu wa Serikali Lakini hali ya Kuzomea Iliendelea Ndipo Mwenyekiti wa Bunge Hilo Alipolazimika Kuliahirisha Bunge Hilo Mpaka Kesho na Kuamuru Mabadiliko hayo Yapelekwe kwenye Kamati Ya Kanuni


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...