WEMA NA AUNT EZEKIEL WATIA KINYAA...!!SHUKA NAYO HAPA...

Uchafu! Picha za madiva wakubwa wa filamu Tanzania, Wema Isaac Sepetu na Aunt Ezekiel Grayson zimebambwa na gazeti hili hivi karibuni wakiwa katika hali ya kimalavidavi licha ya kwamba, mmoja ni mke wa mtu, mwingine mchumba.
Kwa mujibu wa mnyetishaji wetu, ishu hiyo ilichukua nafasi maeneo ya Mikocheni jijini Dar es Salaam ambako Wema na Aunt wamepiga kambi kwa ajili ya filamu yao mpya ya Familia.
Ilidaiwa kuwa, Wema na Aunt ambao kwa sasa wapo ‘klozdi’ kiasi cha watu kuwa na maswali vipi kuhusu Kajala Masanja, walipiga picha hizo wakidhamiria kuzifuta baada ya kujiona lakini lililotokea si akili zao, picha hizo zikanaswa na paparazi wetu.

Staa wa filamu Tanzania, Wema Isaac Sepetu
Juzi, Amani liliwatafuta kwa njia ya simu wawili hao na kuwauliza nini kiliwatia nguvu hadi kupiga picha hizo ambapo Wema anaonekana akibusu sehemu ya paji la uso la Aunt huku naye akiwa amelegeza macho kusikilizia.
Wema: “Unajua huyu Aunt ni mtu ambaye tumezoeana kupita kiasi, tunapomaliza kufanya kazi, tunaanza utani. Halafu kwetu mbona mabusu ni ishu ya kawaida sana!”
Habari za ndani zinasema, baadhi ya ndugu wa mume wa Aunt, Sunday Dimonte wamekuwa wakimtumia meseji ‘mista’ huyo kumweleza uchafu mbalimbali anaofanya mume wake licha ya kutotoa tamko lolote.
Diva wa filamu za kibongo Aunt Ezekiel
Mbali na Dimonte, baadhi ya watu waliozungumza na Amani walimtaka Nasibu Abdul ‘Diamond’ kukaa chini na kufikiri upya kuhusu uamuzi wake wa kumuoa Wema. Wengi wanaamini si sahihi kwake kwa vile haonekani ‘kutulia’ licha ya kwamba wote ‘hawajatulia’


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...