HATARI NIAJE: USIYOYAFAHAMU KUHUSU WAPENZI WEMA SEPETU NA DIAMOND PLATINUMZ...!

Haina ubishi kua Diamond na Wema ndio wasanii pekee wanaoongoza kwa kuandikwa na magazeti na mtandaoni. Wote wawili wanakubalika sana ukianza na Diamond katika mziki na Wema katika Bongo Movie. Usisahau kua Diamond nae kaingia katika Bongo Movie na kaigiza na Wema movie ambayo hadi leo bado inasubiriwa kwa hamu kubwa.
Kama utakua ni mpenzi wa Instagram naamini utakua umewafollow Wema na Diamond kwani ndo watu wanaongoza kwa kuongelewa sana Insta na pia ndio wenye followers wengi zaidi kuliko watanzania wengine wote waliopo katika Instagram. Mpaka Tunaandika habari hii Diamond alikua na followers 120,563 na Wema akmfuatia akiwa na Followers 111,450.  
Unaweza ukaona ajabu kuhusu hili kwani ukweli ni kwamba pamoja na kuwa Diamond na Wema ni wapenzi lakini hakuna aliyemfollow mwenzake kwenye Instagram. Nahisi kila mtu kauchuna akisubiria mwenzake aanze kumfollow.
Kwa upande wa Wema kwenye ndugu zake Diamond kamfollow Queen Dalene tu huku akiacha kuwafollow Halima Kimwana na Esma ambao inasemekana kuwa hawapendi Diamond awe na Wema.  
Diamond yeye ana mawazo tofauti kidogo na Wema yeye kawa Follow ndugu wa Wema wote. Maswali makubwa ni:  Je,ni sawa Diamond kutomfollow Wema Instagram huku Profile picha yake ikiwa ni ya wao wawili?????? Na je, ni sawa kwa Wema kupotezea kumfollow mume wake mtarajiwa??


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...