Home »
Uncategories »
DIAMOND PLATINUMZ AKABIDHI iPAD KWA MSHINDI WA NGOLOLO
DIAMOND PLATINUMZ AKABIDHI iPAD KWA MSHINDI WA NGOLOLO
Unknown
5:25 PM
Msanii
mahiri wa muziki wa kizazi kipya Nasibu Abdul 'Diamond Platinumz'
akimkabidhi iPad yenye thamani ya shilingi milioni 1.2 mshindi wa dansi
ya Ngololo Bw. Faudhu Kiobya kupitia ukurasa wa kijamii wa Instragram wa
Vodacom Tanzania, mara baada ya kumalizika droo ya tatu ya shindano la
miito ya simu. Washindi 35 kila mmoja amejishindia Sh 50,000.
Anayeshuhudia katikati ni Meneja wa huduma za ziada wa Vodacom Bw.
Mathew Kampambe.
Mshindi
wa dansi ya Ngololo Bw. Faudhu Kiobya, aliyejishindia Ipad kwa kutuma
video katika ukurasa wa kijamii wa Instragram wa Vodacom Tanzania,
akionesha iPad
yake kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) baada ya kukabidhiwa
rasmi na Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya Nasibu Abdul 'Diamond
Platinum' (kulia) wakati wa droo ya tatu ya shindano la miito ya simu,
ambapo washindi 35 kila mmoja wamejishindia Sh 50,000. Katikati ni
Meneja wa huduma za ziada wa Vodacom Bw. Mathew Kampambe.
Diamond Platinum (kushoto) pamoja na Meneja wa huduma za ziada wa
Vodacom Bw. Mathew Kampambe, (kulia) wakionyeshwa kurasa mbalimbali
katika iPad na mshindi wa dansi ya Ngololo Bw. Faudhu Kiobya.