Huko Ubungo maziwa kuna ukatili wa kijinsia unaoendelea. Yaani huwa kuna imani kuwa vitendo vingi vya ukatili vinafanywa na wanaume, ila la hasha hata wanawake nao ni balaa. Sababu kubwa ya kuamini hivyo ni ile hali ya kuchukulia unaujua uchungu wa kuzaa, unajua hata wewe hutapenda mwanao afanyiwe vitendo ambavyo sio vizuri, nimekutana na mama huko Ubungo maziwa akiwa amemuajiri mtoto mdogo wa miaka 8 kama house girl na mbaya zaidi anampiga vipigo sana sana mpaka kumkata kata na mtoto ana makovu ya vipigo. Haya yote utayapata ndani ya kipindi cha Joyce Kiria Wanawake Live ndani ya EATV.
Huyu ni mtoto aliyeajiriwa kama mfanyakazi wa ndani na mtoto aliyembeba ni moja ya kazi zake za kulea huyu mtoto.
Huyu ndiye mama mwenye nyumba aliyemuajiri huyo mtoto na huwa anampiga sana.
Hapa nikiwa na hawa watoto
majirani na watu mbalimbali walikuwepo eneo la tukio.
Unaweza ukafikiria hawa wanaishi vizuri, Ila huyu mama anampiga sana huyu mtoto.CHANZO JOYCE KIRIA