WAZIRI WA NISHATI NA MADINI AANZA ZIARA KATIKA MKOA WA MOROGORO


Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akizungumza na watendaji wa  shirika la umeme nchini (Tanesco) ikiwa ni pamoja na wadau wa umeme mjini Morogoro kabla ya kuanza rasmi ziara yake kwenye miradi ya umeme.
Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akitoa maelekezo kwa meneja wa Tanesco mkoa wa Morogoro Deogratius Ndamugoba mara baada ya kujionea moja ya transfoma iliyojengwa kwa ajili ya kupeleka umeme katika kijiji cha Matombo kilichopo katika wilaya ya Morogoro Vijijini.
Kazi ya kuweka umeme ikiwa ni pamoja na kufunga mita ikiendelea kwenye moja ya nyumba zilizopo katika kijiji cha Mtombozi kilichopo katika wilaya ya Morogoro Vijijini.
 Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akizungumza na wakazi wa kijiji cha Mtombozi kilichopo katika wilaya  ya Morogoro Vijijini wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya miradi ya umeme.
 Meneja wa Tanesco mkoa wa Morogoro Deogratius Ndamugoba akitoa  ufafanuzi wa maendeleo ya miradi ya umeme katika kijiji cha Mtombozi mbele ya Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo. 
 Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akisalimiana na mmoja wa wakazi wa kijiji cha Ngong’oro kabla ya kusikiliza kero zao ikiwa ni pamoja na kuzungumza nao
Mwenyekiti wa kijiji cha Ngong’oro Mahamba Shukuru  akiwasilisha changamoto katika upatikanaji wa huduma ya umeme katika kijiji hicho kwa Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter  Muhongo ambapo Waziri huyo ameahidi kufanyia kazi mara moja kupitia kwa watendaji wake. 


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...