Kwa wasiofahamu, Whatsapp ni moja ya programu za simu za mkononi 
inayokuwezesha kutuma ujumbe wa simu kupitia kwenye Intaneti badala ya 
ujumbe mfupi (sms). Kwa kutumia Whatsapp, ina maana utaepuka gharama za 
sms huku ikiwa imesheheni matumizi mengine mengi zaidi kama kutuma 
picha, sauti uliyojirekodi, nk.
Hadi sasa, Whatsapp ina watumiaji hai milioni 450 kila mwezi kutoka
 nchi nyingi duniani, huku kukiwa na watumiaji wapya zaidi ya milioni 
moja kila siku. Hivyo, ni dhahiri kuwa Whatsapp ni programu pendwa na 
yenye kutumika.
Whatsapp inaweza kutumika kama njia rahisi zaidi ya mawasiliano kwa
 watu binafsi na hata makampuni
