
Waziri
 wa Elimu na Mafunzo ya Amali wa Zanzibar Mheshimiwa Ali Juma Shamhuna 
mara alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Muscat kuanza 
Ziara ya kikazi nchini Oman, kushoto ni Waziri wa Elimu ya Juu wa Oman 
Mhe. Dr. Rawiyah Al Busaidi, wa kwanza kulia ni Mheshimiwa Ali Ahmed 
Saleh, Balozi wa Tanzania nchini Oman.
Waziri wa Elimu na 
Mafunzo ya Amali wa Zanzibar Mheshimiwa Ali Juma Shamhuna wa pili kutoka
 kushoto akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Elimu ya Juu wa Oman Mhe. 
Dr. Rawiyah Al Busaidi, wa pili kulia , wa kwanza kushoto ni Mheshimiwa 
Ali Ahmed Saleh, Balozi wa Tanzania nchini Oman.
Waziri wa Elimu na 
Mafunzo ya Amali wa Zanzibar Mheshimiwa Ali Juma Shamhunawa tatu kulia 
akiongoza ujumbe wa Zanzibar katika mazungumzo na Waziri wa Elimu ya Juu
 wa Oman Mhe. Dr. Rawiyah Al Busaidi akiongoza ujumbe wa Oman Kushoto , 
wa nne kushoto ni Mheshimiwa Ali Ahmed Saleh, Balozi wa Tanzania nchini 
Oman.
Waziri wa Elimu na 
Mafunzo ya Amali wa Zanzibar Mheshimiwa Ali Juma Shamhuna kushoto na 
Waziri wa Elimu ya Juu wa Oman Mhe. Dr. Rawiyah Al Busaidi wakitia saini
 nyongeza katika mkataba wa ushirikiano wa Elimu ya Juu baina ya Oman na
 Zanzibar.
Waziri wa Elimu na 
Mafunzo ya Amali wa Zanzibar Mheshimiwa Ali Juma Shamhuna kushoto akiwa 
katika Mazungumzo na Waziri Kazi wa Oman kuhusu ushirikiano katika sekta
 ya mafunzo ya amali.
Waziri wa Elimu na 
Mafunzo ya Amali wa Zanzibar Mheshimiwa Ali Juma Shamhuna kushoto akiwa 
na Mheshimiwa Ali Ahmed Saleh kulia , Balozi wa Tanzania nchini Oman 
alipotembelea Ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Oman pichani chini 
maafisa wa ubalozi na ujumbe wa mheshimiwa waziri wakifuatilia 
mazungumzo.

Waziri
 wa Elimu na Mafunzo ya Amali wa serikali ya Zanzibar Mheshimiwa Ali 
Juma Shamhuna, alifanya ziara ya Kikazi nchini Oman kuanzia tarehe 16 
hadi 20 February 2014 kwa Mwaliko wa mwenyeji wake Mheshimiwa Dr. 
Rawiyah Al Busaidi, Waziri wa Elimu ya Juu wa Oman.
Ziara hii ilikuwa na madhumuni makuu ya kuimarisha uhusiano wa 
kindungu uliopo baina ya Oman na Tanzania kupitia sekta ya Elimu na 
kuimarisha uhusiano wa karibu na ushirikiano baina ya taasisi za elimu 
kati ya Tanzania na Oman.
Katika ziara hii Mhe. Ali Juma Shamhuna alikutana na kufanya 
mazungumzo na Mwenyeji wake Dr. Rawiyah Al Busaidi ambapo pia walitia 
saini nyongeza katika Mkataba wa Mashirikiano katika Elimu ya Juu baina 
ya Zanzibar na Oman . Mheshimiwa Waziri Shamhuna pia alikutana na Waziri
 wa Elimu wa Oman Mheshimiwa Dr. Madihana Ahmed Al Shibaniya na Waziri 
wa Kazi wa Oman Mheshimiwa Abdullah Nassor Al Bakri, .
Mbali na kukutana na viongozi hawa wa Oman, Mheshimiwa Waziri 
Shamhuna alipata nafasi kutembelea maeneo kadhaa kujonea shughuli 
mbalimbali za Taasisi zinazoshughulika na elimu za Oman, alitembelea 
makumbusho ya Jeshi la Oman, Chuo cha Ufundi na Teknolojia, chuo kikuu 
cha Sultan Qaboos na Baraza la Taifa la Utafiti.
Katika maeneo yote aliyotembelea Mheshimiwa Waziri Shamhuna 
alifurahishwa sana na shughuli za taasisi za elimu Oman na kuridhika na 
hatua iliyopigwa na Oman katika sekta ya Elimu na mafunzo ya Amali. 
Mheshimiwa Waziri Shamhuna pia alitembelea ofisi za Ubalozi wa Tanzania 
nchini Oman kujionea shughuli mbalimbali za Ubalozi na pia kuhudhuria 
hafla ya chakula cha Usiku kilichoandaliwa kwa heshima yake nyumbani kwa
 Mheshimiwa Balozi Ali Ahmed Saleh, Balozi wa Tanzania nchini Oman.
CHANZO: MUHIDIN MICHUZI





