ETI HILI NALO NI JINA LA MGAHAWA HUKO GEITA..!! KWELI MAJANGA

Ni siku kadhaa tu zimepita toka mtandao huu ulipofanya matembezi huko Mkoani Geita, lakini baada ya kufika Maeneo ya Bukoli mjini mwandishi alikutana na Mgahawa huu ulioandikwa "TULIA UZAE CAFE" mama huyo anaeonekana katika picha akiendelea kuwahudumia wateja.

Ni maoni yangu tu! kiukweli kwa mtu mwenye heshima zake akitafakari itamuwia vigumu sana kuamua kuingia na kuagiza chochote katika mgahawa huu kutokana na kwamba jina hili  halijakaa kibiashara.

Maoni: kwa wafanyabiasha kiukweli mnatakiwa kuwa wabunifu wa majina ya maeneo ya biashara zenu lakini sio ubunifu huu kwani hii inaweza kuchangia kukosa aina fulani ya wateja haswa wale wanaojitambua.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...