Waziri
 Prof. Mark Mwandosya ametoa taarifa bungeni mjini Dodoma kuhusu ajali 
ya helkopta iliyomkumba makamu wa rais Dkt. Mohamed Gharib Bilal na 
ujumbe wake jana na kusema wamepata majeraha madogo madogo lakini si ya 
kutisha. 
Prof.
 Mwandosya amesema ni jambo la kumshukuru Mungu kuwa wote waliokuwa 
kwenye helkopta hiyo wamenusurika kifo na wapo salama salimini. 
Amesema
 maeneo mengi ya nchi yamekumbwa na maafa ikiwemo Dar es salaam, Pwani, 
Morogoro na mikoa mingine yamekumbwa na mafurikio ikiwemo kuharibika kwa
 miundombinu hasa ya barabara na serikali imeshaanza jitihada za 
kuhakikisha miundombinu hiyo inatengenezwa mara moja na kurudi katika 
hali yake ya kawaida. 
Pia
 waziri Mwandosya amependekeza posho ya leo ya wabunge wa bunge maalum 
la katiba kujitolea posho ya leo ili iwe maalum kwa waathirika wa 
mafuriko sehem mbalimbali za nchi. 
Baada
 ya kuwasilisha taarifa hiyo Mwenyekiti wa bunge maalum la katiba Mh. 
Samwel Sitta amesema suala hilo litaenda kujadiliwa kwenye kamati maalum
 ambayo ina kikao chake leo na itatoa taarifa kwa bunge mara baada ya 
kujadili

