1. Paul Pogba-kiungo wa Ufaransa, miaka 21.
Pogba 
akiwa bado ana miaka 21 amekuwa jasiri ndani na nje ya uwanja. Wengi 
walishangaa kumuona kiungo huyo akipanda kiwango chake kwa kasi 
alipoondoka Manchester United na kujiunga na Juventus mwaka 2012 kwa 
lengo ka kutafuta namba katika kikosi cha kwanza.
Amekuwa 
shujaa wa Claudio Marchisio katika sehemu ya kiungo kwenye ligi ya Seria
 A msimu uliopita na aliichezea Ufaransa mechi ya kwanza ya kirafiki ya 
kimataifa machi 2013 dhidi ya Georgia.
Mwezi 
Julia mwaka huo huo alifanya kazi kubwa kuisaidia timu ya taifa ya 
Ufaransa chini ya miaka 20 katika fainali za kombe la dunia, haikuwa 
rahisi kwa Ufaransa kwenda kombe la dunia bili kijana huyu mahiri.
Umahiri 
wa Pogba amempatia nafasi ya kucheza timu ya taifa na taarifa nzuri ni 
kwamba atakuwa huru nchini Brazil kutoa mchango wake kama alivyofanya 
nchini Italia. Kuwepo kwa Yohan Cabaye na Blaise Matuidi katika safu ya 
kiungo kutamruhusu Pogba kusogea mbele safu ya ushambiliaji.
Frederic 
Lipka, ambaye ni mkurugenzi wa kituo kilichomlea Pogba cha Le Havre 
kabla ya kwenda England, alisema mwaka 2010 kuwa kijana huyo yuko vizuri
 kiufundi kuliko hata Patrick Vieira wakati akiwa na umri kama wake. 
Kwasasa tunasubiri kuona alimaanisha nini.
2. Joel Veltman- Beki wa kati wa Uholanzi, miaka 22.
Habari 
njema kwa beki huyu wa Ajax ni kwamba; kocha mkuu wa Uholanzi Van Gaal 
ameamua kumpa nafasi katika kikosi chake kinachotumia mfumo wa 4-3-3.
Van Gaal 
alimpa nafasi ya kuichezea Uholanzi kwa mara ya kwanza katika suluhu ya 
bila kufungana na Colombia mwezi novemba mwaka jana.
Veltman 
ni mchezaji kijana wa Ajax, lakini hajulikani kirahisi. Namna 
anavyocheza na kimiliki mpira, uwezo wa kupiga mashuti na pasi ndefu 
kunaonesha kama amekaa muda mrefu katika kikosi hicho. Kiukweli alicheza
 mechi yake ya kwanza wiki chache baada ya msimu wa ligi kuu wa 
2011-2014 kuanza na kutulia zaidi. Katika msimu mzima amejiimarisha na 
kuwa chaguo la kwanza la Ajax.
Siku si 
nyingi anaweza kufanya hayo kwa taifa lake, Mfumo wa kulinda kuanzia 
safu ya ulinzi unaopendelea Van Gaal unahitaji wachezaji wanaobadilika 
na kuweza kuusoma mchezo na kucheza vizuri. Hii kazi yote ni ya Veltman 
na anaimudu vizuri.
Pia Van 
Gaal anapenda kuona mpira unakwenda mbele. Kwa maana hiyo Veltman 
anaonekana ndiye chaguo sahihi kuelekea fainali za kombe la dunia mwaka 
huu. Tusubiri kuona beki huyu atafanya nini?.
3. Bernard, Kiungo wa Brazil, miaka 21.
Kwa bei 
yake ya paundi milioni 25, Bernard alizikimbiza timu nyingi wakati akiwa
 katika klabu yake ya Atletico Mineiro mwaka jana. Lakini Shakhtar 
Donetsk walijikaza kisabuni na kuinasa saini ya kiungo huyo majira ya 
kiangazi mwaka jana. Walimpokea vizuri na kuikarimu sana familia yake 
baada ya kuwasili Ukraine. Licha ya Bernard kuzoea kwa taratibu maisha 
ya soka nje ya Marekani kusini, Shakhtar wanaamini jitihada zao za 
kumnasa zilizaa matunda.
Bernard 
anacheza mpira wa kasi, anapenda kutanua uwanja kulia na kuingia eneo la
 namba 10. Mpaka sasa ameanza mechi tatu tu za kimataifa kati ya 10 
alizocheza , na anaonekana atatumika pia msimu huu wa kombe la dunia.
Mbali na 
wengi kumdharau kwa urefu wake wa futi 5 na inchi 6 na uzito wa kilo 63,
 Bernard amekuwa akionesha kiwango cha ajabu. “Shakhtar hawataki 
kuniachia kwa sssa.” Alionya katika mahojiano ya karibuni na O Globo 
baada ya Asernal na Tottenham kutangaza tena nia ya kumtaka .
Sasa tunasubiri kuona maajabu yake katika fainali za kombe la dunia mwaka huu katika ardhi yake.
4. Mattia Destro –mshambuliaji wa Italia, miaka 23.
Mambo yalienda tofauti kidogo. Destro angeletwa katika ulimwengu wa soka na José Mourinho.
Alikuwa 
mfungaji wake wakati Mourinho akiwa Milan. Mshambuliaji huyo alikuwa 
katika kikosi kilichotwaa ubingwa wa UEFA, hata kama hakucheza mechi 
yoyote.
Baada ya 
Mourinho kuondoka, Destro aliuzwa katika klabu ya Genoa, japokuwa 
alianza kuongeza kasi ya kiwango chake baada ya kujiunga na Siena mwaka 
2011.
Kiwango 
chake kiliwavutia zaidi Roma na kumsajili kwa dau zuri-lakini kuingia 
kwa kocha Rudi Garcia katika klabu hiyo kumemweka katika kiwango kikubwa
 zaidi na kuiteka dunia.
Destro 
amekuwa mshambuliaji bora anayesifiwa na kocha wake, huku akimuelezea 
kama “mshambuliaji aliyekamilika”. Hakuna utata wa namba kwake. Katikati
 ya mwezi aprili mwaka huu alifunga bao lake la 13 katika ligi ya seria 
A, huku magoli yake mengi akifunga dakika za mwisho za 85 kwenye michezo
 mingi. Kwasasa kwenye ligi kubwa barani Ulaya hakuna mwenye rekodi ya 
mabao ya aina hiyo.
Destro 
anafunga kila aina ya goli: amekuwa akipiga mashuti ya mbali na karibu. 
Anaweza kuwa chaguo la kwanza katika fainali za kombe la dunia, lakini 
kiwango chake kitamuokoa kwasababu ana upinzani mkubwa kutoka kwa Pablo 
Daniel Osvaldo.
5. William Carvalho , kiungo wa Ureno miaka 21
Sporting 
Clube de Portugal ni akademi kubwa kwa soka la vijana, lakini William 
Carvalho ni ushahidi kuwa baada ya kituo hicho kuwakuza nyota wakubwa, 
Cristiano Ronaldo na Luis Figo, sasa kinamleta nyota huyo mwenye miaka 
21 anayeonekana kuwa kiungo bora zaidi wa Ulinzi na amekuwa na kiwango 
kikubwa mno katika klabu ya Lisbon baada ya kurudi katika klabu hiyo 
akitokea katika mkataba mrefu wa mkopo kwenye klabu ya Cercle Brudgge.
Kujituma 
na kuwajibiki wa Carvalho kulimfanya apewe nafasi ya kucheza kwa mara ya
 kwanza katika mechi ya “play-off” kuwania kombe la dunia dhidi ya 
Sweden mwezi novemba mwaka jana.
Pia 
alicheza kwa dakika zote dhidi ya Cameroon mwezi machi mwaka huu katika 
mechi ya kimataifa ya kirafiki na kujihakikishia namba katika kikosi cha
 kwanza.
Jambo 
jema kwa kocha Paulo Bento ni kuwa nyota wa Porto, Fernando, mzaliwa wa 
Brazil, tayari amepata kibali cha kuichezea Ureno, lakini kutokea kwa 
Carvalho kunaweza kumfanya asimuhitaji tena.
Manchester
 United wamekuwa katika mawindo ya kumnasa Carvalho na ada inayotajwa ni
 paundi milioni 30. Bento ni kocha mwenye maamuzi magumu, haitashangaza 
kuona anamuanzisha Carvalho katika mchezo wa ufunguzi wa kombe la dunia 
dhidi ya Ujerumani.
6. Mario Götze-kiungo mshambuliaji wa Ujerumani, miaka 21.
Ni 
mchezaji ambaye aliwashitua wengi baada ya kutolewa tangazo mwezi aprili
 2013 kuwa anaondoka Borussia Dortmund na kujiunga na wapinzani wao 
Bayern Munich. Mashabiki wa Dortmund waliumia sana kwasababu waliamini 
nyota huyo kijana angekuwa msaada mkubwa kwa Jurgen Klopp.
Inawezekana
 Gotze aliondoka kwa sababu ya presha ya kutaka kuvunja rekodi ya kuwa 
mchezaji ghali zaidi kijana kuwahi kutokea nchini Ujerumani akiwa na 
miaka 21. Dau la paundi milioni 37 lilikuwa kubwa sana kwake. Mashabiki 
walichukizwa na kitendo cha yeye kuondoka, lakini maslahi ndio ilikuwa 
sababu .
Gotze ni 
mtulivu ndani na nje ya uwanja, na alidhihirisha hilo baada ya kufunga 
bao la kuongoza la Bayern Munich aliporejea katika uwanja wake wa Signal
 Iduna Park dhidi ya timu yake ya zamani ya Dortmund mwezi novemba mwaka
 jana.
Kwenye 
mashindano makubwa ya karibuni, Ujerumani wameshindwa kuonesha cheche 
kali na mwaka huu wanahitaji `wauaji` wakali, matarajio yao yapo kwa 
Gotze mwaka huu. Wanategemea miujiza yake ya soka, uwezo wake wa kupiga 
chenga na kasi yake ya `umeme` na uwezo wa kufunga vinawapa matumaini 
makubwa sana Ujerumani.
Hii 
ilionekana wakati alipofunga bao moja la mwisho katika mechi ya 
kimataifa ya kirafiki dhidi ya Chile baada ya kupokea pasi murua kutoka 
kwa Mesut Ozil, ikiwa ni bao lake la saba . Wengi wanaamini nyota wa 
Asernal, Ozil atakuwa msaada mkubwa kumpikia mambo Gotze ambaye kuanza 
kwake katika kikosi cha Bayern Munich msimu uliopita kulimweka matatani 
Frank Ribery. Ujerumani wana bahati ya kuwa na mchezaji muhimu kama 
yeye. Ngoja tusubiri kuona atafanya nini Brazil mwezi ujao.
7. Aleksandr Kokorin, Mshambuliaji wa Urusi, miaka 23
Huyu ni 
kijana mwenye miaka 23 anayekiongoza kizazi cha soka la Urusi kwa sasa. 
Ni rafiki wa vyombo vya habari, anashirikiana na anapatikana mara 
nyingi-lakini mbali ya hayo hapo juu ana kipaji kikubwa mno cha soka. 
Anzhi kwasasa wanafikiria kumuuza kwa paundi milioni 19, lakini 
wanamuuza moja kwa moja katika klabu yake ya zamani ya Dinamo Moscow 
kabla ya kucheza mechi yake ya kwanza.
Kokorin 
ni mchezaji mwenye akili ya mpira, mjanja na amekuwa mmaliziaji mzuri 
msimu wa karibuni. Aliifungia Urusi baadhi ya mabao muhimu yaliyowapa 
tiketi ya kwenda Brazil (alifunga mabao manne katika mechi saba 
alizoanza).
Urusi 
chini ya Fabio Capello wapo kundi moja na Ubelgiji, Algeria na Korea 
kusini na watapata faida ya kumtumia nyota huyu mwenye kipaji cha juu.
Urusi 
wanaamini kuwa nyota huyu atakuwa na ushirikiano mkubwa na mzoefu 
Aleksandr Kerzhakov katika safu ya ushambuliaji. Hii ilionekana wazi 
katika mechi ya kirafiki ya kimataifa ambayo Urusi ilishinda dhidi ya 
Armenia mwezi machi mwaka huu. Hakuna kingine zaidi ya Urusi kusubiri 
furaha kutoka kwa kijana huyu.
8. Mateo Kovacic, kiungo wa Croatia, miaka 19
Ili 
kudhihirisha kuwa Croatia imebarikiwa kuwa na viungo mafundi kama Luka 
Modric Robert Prosinecki na Zvonimir Boban, sasa Mateo Kovacic mwenye 
miaka 19 ni ujio mpya katika kikosi cha nchi hiyo na atacheza pamoja na 
mafundi wengine.
Inahitaji
 ushahidi? anauliza mwalimu wake wa mpira aliyemkuza Niko Kranjcar, 
wakati huo huo naye Boban alikiri kuwa kijana huyo atakuwa mzuri zaidi 
yake enzi za nyuma.
Kumbuka 
Inter walikubali kumnunua kwa dau la paundi milioni 15 kutoka Dinamo 
Zagreb januari mwaka 2013. Makocha wote wawili wa timu hizi alizocheza 
wamehangaika kupata namba yake halali uwanjani. Kovacic amepewe jezi 
namba 10 ya Wesley Sneijder, na hii inatokana na jinsi Inter 
wanavyomthamini wa kipaji chake.
Hajaonesha
 kiwango kikubwa sana katika taifa lake, lakini kijana huyo aliisaidia 
nchi yake kushinda dhidi ya Serbia kuwania kufuzu kombe la dunia 
akicheza kama kiungo wa ulinzi, lakini alionesha soka safi kwenye mechi 
ya “play-off” na Iceland, ambapo alifunga bao kwa kupiga chenga hatari. 
Sasa Brazil inamsubiri.
9. Eden Hazard , kiungo mshambuliaji wa Ubelgiji,miaka 23
Hazard 
amekuwa na kiwango cha juu katika klabu ya Chelsea hata zaidi ya 
alivyokuwa katika klabu ya Lille kwenye msimu wake wa mwisho. Ameongeza 
matumaini makubwa katika nchi yake kuelekea kombe la dunia na inaelezwa 
kuwa hayuko peke yake katika kambi ya Ubelji, wapo wachezaji wengi wenye
 kiwango kikubwa na morali kama yeye.
Hazard 
amekuwa na safari ndefu. Sasa anataka mafanikio zaidi akianza kuitumikia
 Ubelgiji kwenye fainali za kombe la dunia kwa mara ya kwanza akiwa na 
miaka 23 ikiwa ni miaka karibu mitatu imepita tangu alipoichezea nchi 
yake mechi ya kwanza dhidi ya Kazakhstan kuwania kucheza fainali ya Euro
 2012.
Kwasasa 
hakuna shaka kabisa juu ya kuanza kwake katika kikosi cha Ubelgiji. 
Hazard amekuwa akifanya kazi nzuri kutoka winga ya kushoto na katikati, 
japokuwa kufunga mabao mawili tu wakati wa kutafuta tiketi ya kufuzu 
kombe la dunia kulisababisha akosolewe. Lakini bado amedhihirisha uwezo 
wake akiwa na Chelsea ambapo hakuwa na kizuizi tena cha kufunga. Kama 
Hazard ataonesha kiwango kama hicho katika kombe la dunia, basi 
tunatarajia Ubelgiji iwe tishio. 
10. ackson Martinez, mshambuliaji wa Colombia, miaka 27
Hakuna 
mtu nchini Colombia asiyetarajia kuona Radamel Falcao anaimarika zaidi 
kuelekea kombe la dunia baada ya kupata majeruhi makubwa ya goti, lakini
 hata kama atapona, bado atahitaji msaidizi wake.
Mbali ya 
Falcao kuhitaji watu wa kumrithi akiwemo nyota wa Hertha Berlin, Adrian 
Ramos na Teufilo Gutierrez wa River Plate, Jackson Martinez ndiye mwenye
 nafasi kubwa. Akiwa amerithi jezi namba 9 ya Falcao katika klabu ya 
Porto, Jackson amefanya makubwa zaidi kama nyota huyo mwenzake wa 
kimataifa, akifunga magoli 41 katika mechi 53 alizoanza akiwa na Porto 
tangu alipojiunga na klabu hiyo kutokea klabu ya Jaguares mwaka 2012.
Labda 
tuseme anatakiwa kuambiwa juu ya kuzingatia wajibu wake wa kimataifa. 
Martinez alianza katika mechi nne tu za kuwania kufuzu kombe la dunia na
 hakufunga bao lolote. Lakini msimu huu ana njia ndefu baada ya kupewa 
hadhi ya kusimama mbele akiwapiku Fredy Guarin na James Rodriguez.
Jackson 
amekuwa na umbo zuri na uwezo wake wa kufunga sio siri. Amefunga mabao 
muhimu kwa Porto katika mechi za ligi na kimataifa. Nyota huyo mwenye 
miaka 27 anaweza kuwa msaada mkubwa kwa Colombia na kurithi mambo ya 
Falcao ambaye hatakuwa fiti sana kutokana na majeruhi.
Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Mtandao
