WATU
 wawili wamefariki dunia mkoani Kilimanjaro katika matukio tofauti, 
likiwemo la mmoja aliyekutwa amekufa akiwa katika basi la Kampuni ya 
Kilenga akiwa safarini kuelekea mkoani Arusha.Kamanda wa 
Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Moita Koka, alisema kuwa mtu huyo 
ametambuliwa kwa jina la Sayuni Joel (53), mfanyabiashara, mkazi wa 
Mwembe, wilayani Same, Kilimanjaro.
Akizungumzia
 mazingira ya tukio hilo, Kamanda Koka alisema Joel alipanda basi hilo T
 398 BAT na kwamba kabla ya kufikwa na mauti, alikuwa akisumbuliwa na 
tumbo na alikuwa akielekea hospitali kupata matibabu.
Alisema Joel aligundulika kuwa amepoteza maisha baada ya gari hilo kuingia katika stendi kuu ya mabasi Moshi.
Maiti yake imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC huku uchunguzi wa chanzo cha kifo hicho ukiendelea.
Katika
 tukio jingine, mkazi wa Kijiji cha Kilema – Kiyou, Kata ya Kilema, 
wilayani Moshi, Martin Michael (45), amekufa baada ya kujinyonga kwa 
kutumia kamba ya chandarua.
Mashuhuda
 wa tukio hilo walisema lilitokea juzi, saa 8 mchana na kudai kwamba 
amefikia uamuzi huo kutokana na kuchoshwa na hali yake kiafya ambayo 
imemfanya kutumia dawa kila mara na kwamba kabla ya tukio hilo aliwahi 
kusikika akilalamikia hali hiyo.
Na Dixon Busagaga, moshi
 

 
