MWENYEKITI WA BARAZA LA MAIMAMU NA WAHUBIRI KENYA AUAWA

Sheikh Mohammed Idris enzi za uhai wake.
Sheikh Mohammed Idris, ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Maimamu na Wahubiri nchini Kenya, ameuawa karibu na msikiti ulio karibu na nyumba yake na watu wasiojulikana leo asubuhi huko Mombasa.
Duru zinasema kuwa alikuwa amepokea vitisho kutoka kwa vijana wenye itikadi kali za kidini na tayari alikuwa ameelezea hofu juu ya maisha yake.
Wahubiri kadhaa mashuhuri wameuawa katika hali ya kutatanisha katika miaka ya hivi karibuni.
Wengine waliuawa kwa madai ya kuwa na uhusiano wa karibu na kundi la wanamgambo la al-Shabaab huku wafuasi wao wakiilaumu serikali kwa mauaji yao, madai ambayo serikali imakanusha.
Marahemu Idris alikuwa ameitaka serikali kukabiliana na baadhi ya watu wenye itikadi kali za kidini ndani ya msikiti hali ambayo ilisababisha baadhi ya waumini kumuita msaliti.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...