NEY WA MITEGO, WEMA SEPETU, AUNT EZEKIEL NA SHILOLE WAPEWA ONYO BUNGENI

Kabla ya kujadiliwa kwa bajeti ya wizara ya afya na ustawi wa jamii ilianza sehemu ya maswali na majibu kuanzia saa tatu asubuhi mpaka saa nne.
Naibu waziri wa habari utamaduni na michezo Juma Nkamia ndio alijibu swali la Catherine Magige kuhusiana na udhalilishaji wa Wanawake unaofanywa kwenye kumbi mbalimbali za starehe Tanzania.
Waziri Nkamia alisema ‘nakubalia kabisa kwamba kumbi za starehe zimekua zikitoa burudani na ajira kwa vijana hapa nchini lakini ndani ya kumbi hizo kumekua na vitendo vinavyofanyika kinyume na maadili ikiwemo udhalilishaji wa Wanawake’



 Katika kukomesha hali hiyo serikali kupitia baraza la sanaa BASATA wamefanya vikao kadhaa na wamiliki wa bendi, maafisa utamaduni, wakuu wa polisi, wamiliki wa kumbi na wanaojihusisha na uchezeshaji wa mtindo wa kanga moja ili kujadili ukiukwaji wa maadili kwenye sanaa
Waziri amesema 
 Pia serikali imeacha kutoa usajili kwa vikundi kama cha kanga moko kwa kuwa uchezaji wake unakwenda kinyume na maadili ya Tanzania na kutoa onyo kwa wamiliki wa kumbi, Wasanii na hata asasi zinazojihusisha na sanaa ambazo hazifati maadili
Amesema 
 Wasanii waliopewa Onyo ni Ney wa Mitego, Shilole, Wema Sepetu, Aunt Ezekiel na kwa upande wa kumbi ni Mama’s and Papa’s lakini pia maonyesho ya urembo ya Miss Utalii yalifungiwa ambapo pia Serikali imeunda kamati ya kitaifa ya kuzuia ukatili na unyanyasaji dhidi ya Wanawake/Wasichana watoto


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...